NAIROBI, KENYA.
________________
________________
Naibu Waziri Mkuu Uhuru Kenyatta,
Mkuu wa utumishi wa Umma Francis Muthaura na aliyekuwa mkuu
wa polisi Jenerali Hussein Ali watafika mbele ya mahakama ya kimataifa ya
jinai iliyoko the Hague Uholanzi ICC.
________________________________________________
![]() |
| Uhuru Kenyatta |
Viongozi hao wanatuhumiwa kupanga ghasia za baada ya
uchaguzi wa mwaka 2007 nchini Kenya.
Zaidi ya watu 1,000 waliuawa na wengine 500,000 walilazimika
kuhama makaazi yao.
Mahakama hiyo inaanza kupokea ushaidi kuthibitisha ikiwa
watu hao watafunguliwa mashtaka ya uhalifu wa kivita. Viongozi wanaofika
mahakamani leo ni washirika wa karibu wa Rais Mwai Kibaki.
Ghasia zilizuka baada ya wafuasi wa Rais Mwai Kibaki
kutuhumiwa kujaribu kuvuruga uchaguzi wa urais.
Ghasia hizo zilimalizika wakati Bw Kibaki na hasimu wake
Raila Odinga kukubaliana kugawana madaraka, huku Raila Odinga akiwa Waziri
Mkuu.
Kulingana na mwandishi wa Shrika la Utangazaji la Uingereza
(BBC) mjini the Hague Peter Musembi, mwendesha mashtaka Louis Moreno Ocampo
atawasilisha ushaidi wa watu kumi ambao wanasema Bw Kenyatta na Bw Muthaura
walipanga mikutano na kundi haramu la Mungiki ilikuandaa mashambulizi ya
kulipiza kisasi.
Naibu Waziri Mkuu, ameamua kutoa ushaidi wake mwenyewe na
atahojiwa na mawakili wa pande zote.
Kwa upande wake mkuu wa utumishi wa umma Francis Muthaura na
aliyekuwa kamishna wa polisi wanapinga kesi hiyo dhidi yao kwa misingi kuwa
mahakama hiyo haina uwezo wa kuwafungulia mashataka.
![]() |
| William Ruto |
Waziri wa zamani wa Elimu ya juu Wiliam Ruto, waziri wa
zamani wa Viwanda Henry Kosgey na mtangazaji wa redio Joshua Arap Sang ni
washukiwa wengine ambao walihusishwa na chama cha waziri mkuu Raila Odinga.
Washukiwa hao walifika mahakamani mapema mwezi huu kujibu
mashtaka ya kupanga ghasia hizo na kusababisha maafa hayo.
_____________________________________________________________
Reuters/BBC


No comments:
Post a Comment